Uncategorized

SHULE 18 ZAFUNGIWA NA SERIKALI KIGAMBONI

Posted on

Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni imeendesha zoezi la kufunga shule za msingi na awali ambazo hazina usajili katika manispaa hiyo.
Zoezi hilo limesimamiwa na Kaimu Afisa Elimu wa Manispaa ya Kigamboni, Mwalimu Mathew Komba pamoja na Wakaguzi wa Elimu katika manispaa hiyo.
Image result for WANAFUNZI
Katika zoezi la ukaguzi katika shule mbalimbali, mapungufu mbalimbali yalipatikana ambayo ni pamoja na shule kutokuwa na usajili,
madarasa machache, kutokuwa na vyoo kwa ajili ya wanafunzi na walimu ambapo baadhi ya shule zinatumia vyoo vya misikiti au wanafunzi kujisaidia kwenye vyoo vya jirani .
Katika siku ya kwanza ya ukaguzi huo, timu hiyo imezifunga shule 18 kati ya 58 zilizobainishwa kutokuwa na usajili katika kata za Kigamboni, Vijibweni na Tungu.
Kati ya shule zilizofungwa ni Malaika Nursery School, Kigamboni English Medium School, Patmos, Montecarlos, Riziki, Taqwa, Firdaus na Meck.
Aidha, uongozi wa Manispaa ya Kigamboni imewataka wazazi kutowapeleka watoto wao kwenye shule hizo mpaka hapo watakapokimilisha taratibu walizowekewa pamoja na kupata usajili.

from Blogger http://ift.tt/2wyc0Bq
via IFTTT

UKITAKA KUSTAAFU MAPEMA ZINGATIA MAMBO HAYA.

Posted on

  • Watu wengi sana wanatamani kuwa na uwezo na uhakika wa kustaafu mapema, lakini ni wachache sana wanachukua hatua mahususi kuhakikisha wanalitimiza jambo hilo.
  • Ili uweze kustaafu mapema, mambo matatu yanahitajika: kipato cha uhakika, kuweka akiba na kuwekeza akiba yako.
  • Jambo la kuzingatia ili utimize lengo hili ni kufanya mambo hayo matatu yawe ndio kipaumbele chako maishani.
  • Vijana wanajulikana kwa kuwa na tabia ya kutopenda kufata sheria, na linapokuja swala la matumizi ya pesa zao wanazozipata kwa jasho lao – wengi zaidi huwa hawataki hata ushauri kabisa.

    Lakini uwezekano wa kustaafu mapema unaweza kuwafanya wengi washawishike kuachana na ubishi wao na kufikiria uhakika wa maisha yao ya uzeeni na kuanza kuchukua hatua za uhakika kuyanyoosha wangali bado vijana na wenye nguvu za kufanya kazi.

    Image result for GRAND PARENTS

    Zifuatazo ni njia hizo na jinsi ya kufanya:

    1. Tengeneza chanzo imara cha mapato
    Kama huna chanzo cha mapato, hutakuwa na nafasi hata ya kuanza kujenga utajiri. Hatua ya kwanza kabisa ya kuhakikisha unapata uhuru wa kipato ni kuwa na chanzo cha uhakika cha kipato ili uwe na uhakika kwamba kutokana na kipato hicho, unaweza kuweka akiba pamoja na kuwekeza kwa ajili ya maisha ya baadaye.

    Kwa baadhi ya watu, hii yaweza kumaanisha ufanye kazi kwa ufanisi kwenye ajira yako ya sasa ili uweze kutimiza lengo hili. Ukiwa na chanzo cha uhakika cha mapato, hata ikiwa ni kutokana na kazi za mkataba au tenda za kulipwa kwa siku, bado unaweza kuweka mipango ya baadaye na kuanza kuitekeleza, japo kidogo kidogo.

    2. Weka akiba sehemu kubwa ya kipato hicho
    Ukishakuwa na kipato cha uhakika, jambo muhimu ni kuhakikisha kuwa hutumii pesa yote unayopata. Kujifunza jinsi ya kuishi maisha ya gharama nafuu chini ya kipato chako ni muhimu ili uweze kubaki na pesa (hasa ukianzia ujanani mwako) na uweze kujiwekea akiba itakayokusaidia kwa maisha yako yote yaliyobaki.

    kwanza, miongoni mwa njia rahisi zaidi za kuhakikisha utakuwa na fedha uzeeni mwako ni kujiunga na mfuko wa hifadhi za kijamii. Mifuko hii itakusaidia kutoa michango yako kila mwisho wa mwezi au kwa muda maalum na kuja kuipata utakapotimiza umri wako wa kustaafu. Kwa waajiriwa, michango hii huwa inakatwa moja kwa moja kutoka kwenye mshahara wako – kwahiyo huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu hilo – lakini kwa ambao hawajaajiriwa, unaweza kujiunga kwenye mifuko hii kama mtu binafsi, kwakuwa inaruhusiwa kufanya hivyo pia. Michango unayoiweka ni kiasi kidogo sana cha pesa kwa mwezi, lakini faida yake uzeeni ni kubwa.

    Pia, unaweza kupunguza matumizi yako ya pesa kwa kupunguza gharama za nyumba (kama umepanga) ili kodi yako kwa mwezi isizidi asilimia 30 ya kipato chako.

    3. Wekeza akiba yako kwenye vitega uchumi vitakavyoongezeka au kutopungua thamani
    Kuwa na pesa nyingi kwenye akiba yako ni jambo zuri, lakini unapoiwekeza pesa hiyo yaweza kusababisha tofauti kubwa sana kwenye safari yako ya kustaafu mapema.

    Kuna wanaoamua kuwekeza kwenye sekta ya majumba, na inaweza ukunufaisha kwakuwa una uwezekano wa kuingiza kipato cha kila mwezi kutokana na kodi za pango.

    Kwa wale wasiovutiwa na biashara ya majumba, unaweza kujifunza na kuwekeza kwa kununua hisa za makampuni mbalimbali ambayo yana rekodi nzuri ya ukuaji.

    Mwanzo wa safari ya mafanikio ya kuwa na uhuru wa kipato unaanza kwa uamuzi wako kwamba kufanya hivyo ni muhimu sana kwako. Kisha ukiwa unazingatia malengo yako, basi unaweza kutimiza kila unachokitaka bila wasiwasi.

    from Blogger http://ift.tt/2vYuBW9
    via IFTTT

    ULIPAJI KODI YA ARDHI KWA SIMU ZA MKONONI WAANZISHWA NA SERIKALI

    Posted on

    Ili kujua unadaiwa kiasi gani cha kodi ya pango la ardhi kwa kutumia simu ya mkononi bonyeza *152*00# au kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi yaani SMS halafu unatuma kwenda namba 15200 na baada hapo unaweza kulipia kwa njia ya Mpesa, Tigo Pesa au kulipia tawi lolote la benki ya NMB na CRDB.
    Image result for i phone
    Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ikishirikiana na Wizara ya Fedha, imesambaza maafisa wake katika Halmashauri 169 kote nchini kutoa mafunzo katika vituo vyote vya makusanyo ya kodi ya ardhi na tozo nyingine kwa kutumia simu ya mkononi ili kuondoa kabisa mfumo wa zamani wa malipo.
    Zaidi ya maafisa 170 kutoka makao makuu ya Wizara ya Ardhi, Wizara ya Fedha na kutoka kanda nane za ardhi wameanza kutoa elimu hiyo katika Halmashauri na vituo vyote vya makusanyo ya kodi ya ardhi ili kurahisisha ulipaji kodi ya ardhi kwa wananchi kwa kutumia simu zao na kuondoa usumbufu.
    Mfumo wa ulipaji kodi ya pango la ardhi kwa njia ya simu ya mkononi ni mfumo wa kielektroniki wa Government electronic Payment Gateway (GePG) katika makusanyo ya kodi ya pango la ardhi ambao utamrahisishia wananchi kulipia popote walipo kwa kutumia simu zao kwa urahisi zaidi.
    Mwananchi yeyote anayemiliki kiwanja au shamba lililopimwa na kupatiwa hati, ataweza kutumia simu yake ya mkononi kujua kiasi cha kodi ya pango la ardhi anachodaiwa na kulipa kwa kutumia simu yake ya mkononi.
    Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeanza rasmi kutumia mfumo huu wa kielektroniki wa GePG katika makusanyo ya kodi ya pango la ardhi pamoja na tozo nyingine zinazotokana na sekta ya ardhi nchini na kuondoa kabisa mfumo wa zamani.
    Mfumo huu utamrahisishia mwananchi kulipa kodi ya pango la ardhi popote alipo, ikiwa ni pamoja na kulipia tozo nyingine mbalimbali za sekta ya ardhi. Mmiliki wa kipande cha ardhi ataweza kujua anadaiwa kiasi gani cha kodi ya pango la ardhi na kulipia popote alipo bila kusumbuka kufuata huduma hizo katika vituo vya makusanyo.
    Kwa majaribio ya ukusanyaji kodi ya pango la ardhi kwa kutumia mfumo wa kielektroniki yalifanywa katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani na baada ya mafanikio makubwa kuonekana elimu ikatolewa kwa watendaji wote wa sekta ya ardhi katika Halmashauri zote za mkoa wa Dar es salaam kabla ya zoezi hilo kuhamishiwa mikoani.
    Kwa zile huduma nyingine za sekta ya ardhi ambazo zinahusisha malipo kama vile upekuzi katika daftari la msajili (official search), mwananchi atapaswa kutembelea ofisi za Wizara ya ardhi zilizo katika eneo lake na kupatiwa makadirio ya kulipia huduma husika pamoja na namba ya malipo itakayomuwezesha kulipia aidha kwa njia ya benki au simu ya mkononi.
    Kwa sasa kikosi kazi kinachotoa mafunzo juu ya matumizi ya mfumo huu kimeshaanza kuelemisha mikoa mingine baada ya kupata mafanikio mazuri katika mkoa wa Dar es Salaam. Lengo kubwa la kutumia mfumo huu ni kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa maduhuli ya serikali pamoja na kurahisisha ulipaji kodi ya pango la ardhi nchini.

    from Blogger http://ift.tt/2xsNb6q
    via IFTTT

    MAABARA YA NYUKLIA YAANZA KUJENGWA NASERIKALI

    Posted on

    Serikali imetenga shilingi bilioni 2.3 kwa ajili ya ujenzi wa maabara ya kisasa ya nyuklia katika Tume ya Nguvu za Atomiki (TAEC). Lengo la maabara hiyo ni kutoa huduma bora za kisasa za masuala ya mionzi kwa nchi za Afrika.
    Aidha, vifaa vyenye thamani ya shilingi bilioni 11.5 kwa ajili ya maabara hiyo vilivyotolewa na Umoja wa Ulaya (EU) vimeanza kuwasili nchini na kuhifadhiwa kwenye maabara za tume hiyo.
    Akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa maabara hiyo jana, Waziri wa Elimu, Sayansi, na teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alisema shilingi bilioni 2.3 hizo zimetolewa na Serikali na zimetokana na fedha za ndani.
    Alisema Serikali imetoa kwanza shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo linalotarajiwa kukamilika Februari mwakani. Kiasi kilichobaki cha shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo kitafuatia ili maabara hiyo ya kisasa iweze kutumiwa na watu mbalimbali nchini na Afrika nzima.
    “Tunamshukuru Rais John Magufuli kwa kuwezesha,” alisema Profesa Ndalichako. “Maendeleo ya nchi yanasongwa hasa katika kuhakikisha tume hii inapata maendeleo na kuchangia fedha katika mfuko huu wa Serikali.”
    Akizungumza katika hafla hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAEC, Brigedia Jenerali Fulgence Msafiri, alisema maabara hiyo itatoa huduma mbalimbali za matumizi salama ya mionzi pamoja na kuwa msaada kwa wanafunzi wa vyuo vikuu katika ngazi ya shahada ya Uzamili na uzamivu.
    HT @ Nipashe

    from Blogger http://ift.tt/2wnr704
    via IFTTT

    MAMLAKA YA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA YAVUNJWA NA RAIS MAGUFULI

    Posted on

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 23 Agosti, 2017 amemteua Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi kuwa Kamishna wa Operesheni wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya.
    Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi anachukua nafasi ya Bw. Mihayo Msikela ambaye amerejeshwa Makao Makuu ya Polisi.
    Uteuzi wa Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi unaanza mara moja.

    Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amezungumza na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa Kulevya Bw. Rogers William Siyanga ambaye amemhakikishia kuwa kazi ya kukabiliana na tatizo la biashara na matumizi ya dawa za kulevya inaendelea vizuri.

    Bw. Rogers William Siyanga amesema tatizo la dawa za kulevya lilikuwa kubwa na ametaja dawa za kulevya ambazo Mamlaka inapambana nazo kuwa ni bangi, heroine, cocaine, kemikali bashirifu na kwamba kwa sasa imeanza kukamata na kuharibu mashamba ya bangi na bangi iliyovunwa.

    Amebainisha mikakati mitatu inayotumika katika mapambano dhidi ya tatizo hilo kuwa ni kuzuia dawa za kulevya zisiingie nchini, kutoa elimu kuanzia shule za msingi, sekondari, vyuo na kwenye jamii ili watu waache kutumia dawa za kulevya na kutoa tiba kwa watu walioathirika na dawa za kulevya, na pia ametoa wito kwa watu wenye waathirika wa dawa za kulevya kuwapeleka katika mamlaka hiyo ili watibiwe.

    Gerson Msigwa

    Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

    Dar es Salaam

    23 Agosti, 2017

    from Blogger http://ift.tt/2ipaI5F
    via IFTTT

    Posted on

    KISA CHA NDEGE NDOGO (DRONE) ILIYOPELEKEA MZEE WA GHANA KUHIJI MAKA

    Share this
    Mzee Al-Hassan Abdullah ni mzee masikini anayeishi kijijini nchini Ghana. Hadithi yake ilisambaa sana kwenye mitandao ya kijamii nchini Uturuki baada ya mzee huyo kuwauliza wafanyakazi wa kituo cha runinga cha nchini Uturuki waliokuwa wakirekodi kipindi nchini Ghana iwapo ndege ndogo isiyokuwa na rubani (drone) iliyokuwa inatumiwa na wafanyakazi hao kurekodi “kama ndege hiyo inaweza kumpeleka Makka kuhiji” amesafirishwa kwenda Mji huo Mtakatifu kwa imani ya Uislam kwa gharama za Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki na michango iliyotolewa na raia mbalimbali nchini Uturuki walioguswa na alichokisema Mzee Abdullah.
    Kilichotokea ni kwamba ndege hiyo ilidondoka karibu kabisa na nyumba ya Mzee Abdullah wakati waandishi hao wanarekodi kipindi maalum. Mzee huyu baada ya kuiona ndege hiyo aliiokota na kumsubiri rubani wake aliyekuwa anaifata aichukue. Akiwa anamkabidhi rubani ndege hiyo, ndipo Mzee Abdullah akamuuliza iwapo wana ndege nyingine kubwa zaidi ya hiyo inayoweza kumpeleka mpaka Makka ili akatimize ibada ya kuhiji kama walivyo mamilioni ya waumini wengine watakaohiji mwaka huu. Rubani huyo aliamua kupimga picha mzee huyu na kuandika maneno aliyoulizwa kisha kuituma kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii. Ujumbe huu ulisambaa mara moja na kuwagusa wengi kiasi cha Serikali ya nchi hiyo kuamua kulipia safari yake. Wananchi walioguswa pia waliweza kutoa mchango wao kama sadaka kumuwezesha kwenda kutimiza ibada hiyo.
    Ujumbe wake uliposambaa sana kwenye mitandao ya kijamii nchini Uturuki, Waziri wa Nchi za Nje, Mevlüt Çavuşoğlu aliguswa na kushughulikia safari ya mzee Abdullah ambaye ni masikini wa kutupwa kwenda Makka. Mzee Abdullah aliwasili jijini Istanbul, Uturuki juzi Ijumaa akitokea Accra, Ghana na alipokewa na Shirika la Misaada nchini Uturuki ambalo limelenga kusaidi nchi ya Ghana.

    Mzee Al-Hassan Abdullah: Kushoto alipokuwa anamkabidhi rubani ndege ndogo baada ya kuanguka karibu na nyumba yake Kulia ni katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa Istanbul, Uturuki
    Abdullah aliliambia Shirika la Utangazaji la Anadolu la jijini Ankara, Uturuki kuwa amefurahi kuwa jijini Istanbul na kwamba ni Mungu ndiye aliyembariki kuweza kupata msaada kutoka Serikali ya Uturuki. “Namshukuru Mungu na namuombea kila aliyenisaidia kutimiza ndoto yangu. Msaada wa Serikali ya uturuki ni wa muhimu sana kwangu na ninaamini utakuwa ni uthibitisho wa urafiki kati ya mataifa yetu na kuonesha udugu kwa waislam,” alisema.
    Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya misaada iliyompokea mzee huyu, Cihad Gökdemir amesema kwamba ujumbe wa Mzee Abdullah ulisambaa zaidi kwenye vyombo vyote vya habari nchini humo baada ya mfanyakazi wa kituo hicho cha runinga kuweka picha ya mzee huyo kupitia mtandao wa Twitter. “Hapo ndipo watu wengi walipoanza kuwasiliana na mfanyakazi huyo awaongoze jinsi ya kumsaidia Mzee Abdullah, watu wote – wafanyabiashara hadi makampuni. Mwisho, Ofisa wa Polisi kutoka Ubalozi wa Uturuki nchini Ghana akawasiliana naye. Anawashukuru sana watu wa Uturuki,” alisema Gökdemir.

    from Blogger http://ift.tt/2xkhXhI
    via IFTTT

    KILIMO CHA PARACHICHI NJOMBE

    Posted on

    from Blogger http://ift.tt/2ihQFpI
    via IFTTT

    HII NDIYO KAULI YA SERIKALI KUHUSU WANAFUNZI KWENDA VYUO VIKUU BILA KUHITIMU KIDATO CHA SITA

    Posted on

    Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inapenda kuutarifu umma kuwa taarifa zinazosambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari
    “Serikali yapiga Marufuku Kusoma Shahada bila kupita Kidato cha Sita,” tarifa hiyo siyo ya kweli na haijatolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mh. Joyce Ndalichako.Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako hajatangaza popote na kuwa taarifa hiyo haina ukweli wowote.
    Profesa Ndalichako yuko Mkoani Kigoma kwenye ziara ya ufuatiliaji wa Miradi ya Elimu, inayotekelezwa kwa ushirikiano wa Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara yake.
    Vile vile Wizara inapenda kutoa wito kwa watanzania kuacha kutumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kuupotosha umma kwa taarifa ambazo siyo sahihi na hazina ukweli wowote.
    Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ina utaratibu wake wa kutoa taarifa hivyo inawaomba radhi wale wote waliopata usumbufu kutokana na kusambaa kwa taarifa hiyo.
    Imetolewa na:
    Mwasu Sware
    Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
    WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
    19 Agosti, 2017

    from Blogger http://ift.tt/2vWsuAs
    via IFTTT

    DAR:MENO YA TEMBO YENYE KILO 376 YAKAMATWA NA SERIKALI

    Posted on

    Waziri wa Maliasli na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amesema serikali imefanikiwa kukamata jumla ya meno ya tembo 28 katika ghala moja lililopo Mbezi Beach jijini Dar es salaam, yenye uzito wa takribani kilo 376.
    Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Waziri Maghembe amesema meno hayo yaliyokamatwa tarehe 13 na 14 mwezi wa nane mwaka huu yanaonekana ni ya tembo waliouawa miaka ya nyuma ikikadiriwa kuuawa miaka ya 2013 au 2014 na wahalifu hao kuyaweka majumbani mwao huku wakiendelea kutafuta masoko.
    Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Mghembe akizungumza na waandishi wa habari wakati alipokuwa akiwaonesha jumla ya meno ya tembo 28 yakiwa na takribani kilo 376 yaliyokamatwa kwenye ghala katika eneo la Mbezi Beach hivi karibuni. Jumla ya watuhumiwa wa ujangili wapatao 6 tayari wameshakamatwa akiwemo Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa na Imam wa msikiti wa Huda wa Mbezi Beach, Aboubakar Zuberi Segumi ( Picha na Lusungu Helela- WMU)
    Waziri Maghembe amesema tayari hadi hivi sasa watuhumiwa sita wa ujangili wameshakamtwa akiwemo Mohamedi Yahya Mohamed, almaarufu Mpemba, Aboubakar Zuberi Seguni mkazi wa Mbezi Beach ambaye pia ni mwenyekiti wa serikali za mtaa na imamu wa msikiti wa Huda uliopo Mbezi, Juma Saleh Jebo mkazi wa Manzese jijini Dar es salaam, Hamisi Rashid Omary mkazi wa Mbezi, Amir Bakari Shelukindo Mkazi wa Gairo Morogoro na Ahmed Shabani Bakari mkazi wa Mkuranga.
    Wakati akiwataja watuhumiwa hao, Waziri Maghembe alisema vita dhidi ya ujangili ni ngumu kwa vile hata baadhi ya watu wasiotegemewa katika jamii kujihusisha nayo nao wamo, akitolea mfano wa mtuhumiwa, Bakari Zuberi Seguni mkazi wa Mbezi Beach ambaye pia ni mwenyekiti wa serikali za mtaa na imamu wa msikiti wa Huda uliopo Mbezi kuwa yeye ni mfano katika jamii kwa kuwa ni kiongozi wa kiserikali lakini pia ni mtu wa Mungu ambaye ni ngumu kufikiria ni miongoni mwa washirika wa biashara hiyo haramu.
    Aliongeza kuwa, Tanzania kupitia Wizara yake inataka kufuta kabisa biashara ya meno ya tembo kama China walivyofanya licha ya kuwa uuzaji wa meno ya tembo kwa sasa mara baada ya kufuta soko la wazi imekuwa ikiendelea kwa njia ya mtandao.
    Katika hatua nyingine , Waziri Maghemba alipaza sauti kwa mataifa kama vile Vietnam na Thailand kuacha kujihusisha na biashara hiyo na kuiomba jumuiya ya Kimataifa kuingilia ili tembo waendelee kuwepo kwa faida ya kizazi kijacho na badae na dunia kwa ujumla.
    Aidha, Waziri Maghembe amesema Tanzania na Dunia kwa ujumla imepata pigo kubwa baada ya kutokea kwa mauaji ya Mkurugenzi wa Palm Foundation, Wayne Lotter raia wa Afrika Kusini yaliyotokea usiku wa jana Masaki jijini Dar es Salaam kwa kuwa alikuwa mstari wa mbele katika kuisaidia serikali katika vita dhidi ya Ujangili.

    from Blogger http://ift.tt/2xhCLXd
    via IFTTT